Friday, May 24, 2013
RAIS KIKWETE AKUTANA NA TIMU YA TAIFA IKULU JIJINI DAR LEO
Rais Jakaya Kikwete akiongea na wachezaji wa timu ya mpira ya Taifa, Taifa Stars leo Ikulu jijini Dar es salaam alipokutana nao kuwapa hamasa waweze kupata ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco utakaochezwa Juni 7, na michezo mingine ikiwa ni hatua ya kuiwezesha timu hiyo kukata tiketi ya kushiriki mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014.
Rais Jakaya Kikwete akiwaaga wachezaji wa Timu ya Taifa Stars mara baada ya kukutana nao leo Ikulu Jijini Dar es salaam kuwahamasisha washinde mchezo dhidi ya timu ya Taifa ya Moroco utakaofanyika June 7 ikiwa ni sehemu ya Taifa Stars kutafuta ticketi ya kucheza mashindano ya Kombe la Dunia.
Meneja wa Timu ya Taifa Stars Bw. Mukebesi akiteta jambo na Kepteni wa Timu ya Taifa Stars Juma Kaseja Ikulu jijini Dar es salaam walipokutana na Rais Jakaya Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya Pamoja na wachezaji wa Timu ya Taifa , Taifa Stars, viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo na Viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Taifa , Taifa Stars Ikulu jijini Dar es salaam.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.
Na. Veronica Kazimoto –MAELEZO.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amekutana na timu ya Taifa (Taifa stars) kwa lengo la kuitia moyo katika mechi ijayo kati yake na timu ya Moroco ikiwa ni harakati za Tanzania kutafuta tiketi ya kucheza fainali za kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka 2014.
Rais Kikwete ameiambia timu hiyo kuwa ina uwezo mkubwa wa kusonga mbele kutokana na uwezo mkubwa waliouonesha katika mchezo wao dhidi ya Gambia ambapo walifanikiwa kupata ushindi wa bao 2-0.
“Maadamu mara ya kwanza mliwashinda Gambia, hakikisheni pia mnapata ushindi dhidi ya Moroco, mkishinda tunafurahi sana na mkishindwa tunanyong’onyea sana,” amesema Rais Kikwete.
Aidha amempongeza kocha wa timu hiyo Kim Poulsen pamoja na Kamati ya Taifa ya ushindi ya Taifa stars kwa kuisaidia timu hiyo kiasi cha shilingi milioni 30 ikiwa ni mkakati wa kuiongezea nguvu kwa hatua iliyofikia na kuwataka wachezaji kujituma ili kuwafurahisha watanzania ambao hivi sasa wanaipenda timu yao ya Taifa.
Nae Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fenera Mukangara amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo nchini ili kuondoa changamoto zinazoikabili timu hiyo.
Kwa upande wake Kocha Poulsen, amemshukuru Rais Kikwete kwa kuwakaribisha na kuwatia moyo ambapo ameahidi kuifundisha vizuri timu hiyo ili kuhakikisha kuwa wanapata ushindi.
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake kaptaini wa timu hiyo Juma Kaseja amemshukuru Rais Kikwete na kuahidi kujituma kwenye mazoezi na hatimaye kuibuka washindi kwenye mechi zijazo.
Taifa stars ambayo inakamata nafasi ya pili katika kundi C inatarajia kucheza ugenini na Morocco mnamo Juni 7 mwaka huu.
Thursday, May 23, 2013
MINISTRY OF TOURISM AND TOURISM PRIVATE SECTOR JOINTLY DISCUSSED TOURISM DEVELOPMENT LEV
ONE OF THE REPRESENTATIVE OF TOURISM PRIVATE SECTOR EXPLAINING A POINT TO THE MINISTER OF NATURAL RESOURCES AND TOURISM, HON. KHAMIS KAGASHEKI DURING THE DIALOGUE.
| The Ministry of Tourism and Natural Resources today hosted a dialogue forum with the Tourism Private Sector on the Tourism (Tourism Development levy) Regulations 2012 at Dar es Salaam Serena Hotel. During the dialogue issues that were discussed included:- .Effective partnership for tourism development .Tourism development levy & regulations 2012 as well as .Improving tourism investment - Business environment . |
legal officers discussing that raised during the forum
DROO YA KWANZA YA WINDA NA USHINDE YAFANYIKA LEO JIJINI DAR.
Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo, akiongea na mshindi wa droo ya kwanza ya Winda na Ushinde kwa njia ya simu iliyochezeshwa leo katika ofisi za Kampuni ya bia ya Serengeti jijini Dar es Salaam
Meneja mauzo na masoko wa kampuni ya Push Mobile Media Rugambo Rodney(katikati) akiwaonesha kitu Afisa mwandamizi wa PWC Tumainieli Malisa(kushoto) na Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo(kulia)
Meneja wa Bia ya Serengeti Allan Chonjo (katikati) akizungumza kwa njia ya simu na mshindi wa 1,000,000 wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya Winda na Ushinde leo katika ofisi za Kampuni ya bia ya Serengeti, akiwa pamoja na Meneja mauzo na masoko Rugambo Rodney(kulia) na Afisa mwandamizi wa PWC Tumainieli Malisa(kushoto).
Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo, akimtangaza Honest Minja(38) mshindi wa Tsh 1,000,000 wa droo ya kwanza ya Winda na Ushinde kwa wana habari katika droo iliyochezeshwa leo katika ofisi za Kampuni ya bia ya Serengeti jijini Dar es Salaam.
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA UTOKOMEZAJI WA UGONJWA WA FISTULA, JIJINI DAR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baba wa mtoto, Elizabeth Nora kutoka Dodoma aliyelazwa katika Hospitali ya CCBRT, wakati Makamu alipofika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Dokta wa Hospitali ya CCBRT, wakati alipokuwa akitembelea katika wodi za wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo, alipofika hospitalini hapo leo, kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Kulia ni Mtoto Boniface Patrick akiwa na Baba yake, Patrick Luwao, Wakazi wa Dodoma, akiwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji na kuongezewa sehemu ya mguu uliokuwa mfupi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Stellah Nzyemba, ambaye awali alikuwa mgonjwa na baada ya kutibiwa katika Hospitali hiyo ya CCBRT na kupona ameajiriwa ili kuwasaidia wagonjwa wa Fistula. Makamu alifika hospitalini hapo leo kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea katika Wodi ya wagonjwa wa Fistula, wakati Makamu alipofika hospitalini hapo leo kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula.
Makamu wa Rais Dkt Bilal, akimjulia hali mtoto mgonjwa aliyelazwa katika Hospitali hiyo ya CCBRT
Baadhi ya wasichana waliokuwa wakiugua ugonjwa huo na kutibiwa katika Hospitali ya CCBRT, ambao kwa sasa wanapewa mafunzo ya kufanya kazi za mikono.
Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akiwasili katika eneo lililoandaliwa maalum kwa ajili ya kufanyia shughuli za maadhimisho hayo.Picha na OMR
RAIS Jakaya Kikwete ATHIBITISHIA UMMA KWAMBA PSPF IKO IMARA NA HAITAKUFA
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya
Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake.
Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma. Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji .
Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena.
Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma. Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji .
Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena.
1.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kipeperushi cha nyumba za PSPF
zinazokopeshwa kwa wanachama wa Mfuko huo, huku akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko huo ndugu Adam H. Mayingu
akimuelezea kuhusu nyumba hizo na fursa zingine zilizopo PSPF kwa Watanzania
ikiwa ni pamoja na ujumbe kwa Watanzania kwamba mtu yeyote mwenye umri
usiopungua miaka 18 anaweza kuwa mwanachama wa PSPF
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa
Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr.
Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania
hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la
Ujasiliamali na Elimu.
Mtangazaji wa TBC Amina Mollel
akikabidhi fomu ya kujiunga na PSPF kwa Meneja Masoko wa Mfuko huo Bi.
Costantina Martin mala baada ya kuvutiwa na kukata shauri ya kuwa mwanachama wa
Mfuko wa kwa njia ya uchangiaji wa hiari
Timu ya PSPF iliyokuwa kwenye
maonyesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao ndugu
Adamu Mayingu katikati. Timu hiyo
inastahili pongezi kutokana na uduma bora waliyokuwa wakiitoa kwa wananchi
waliokuwa wakitembelea banda hilo la PSPF pale Nyerere squire Dodoma.
Wanachama
wa PSPF wakipata taarifa mbalimbali ikiwapo historia ya michango yao na taarifa
za uanachama.
mkutano wa kamati ya kitaifa ya wataalam ya mabadiliko ya tabia nchi unaendelea mjini zanzibar.
Bw Sihaba Vuai afisa mazingira ofisi ya makamu wa kwanza wa rais zanzibar akizungumza kuhusu hali ya mazingira na zanzibar na mathara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi katika mkutano wa kamati ya kitaifa ya wataalam ya mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini zanzibar.
|
Wanakamati ya kitaifa ya kitaalam ya mabadiliko ya tabia nchi wakimsikiliza mtoa mada hayupo pichani katika mkutano unaoendelea mjini zanzibar (Picha na Evelyn Mkokoi)
Rais Kikwete amwapisha Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria na Mabalozi Wapya wanne
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais
Dkt.Mohamed Gharib Bilal na Waziri wa
Mambo ya Nje Bernard Membe wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi
wapya
waliopaishwa leo ikulu jijini Dar es Salaam.aliyesimama mbele kushoto no
Balozi
Liberata Mulamula anayekuwa Balozi Mpya wa Tanzania nchini
Marekani.
Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za Maziwa Makuu.(picha na Freddy Maro).

Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za Maziwa Makuu.(picha na Freddy Maro).
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ikulu jijini Dar es Salaam
amemwapisha Jaji Aloycius Mujuluzi kuwa
Mwenyekiti wa tume ya kurekebisha sheria
pamoja na mabalozi wanne watakaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi.Mabalozi
walioapishwa leo ni pamoja na Balozi mpya katika umoja wa Falme za kiarabu(UAE)
Mbarouk Nassor Mbarouk,Balozi mpya wa Tanzania nchini Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi
mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga na Mwakilishi wa kudumu Tanzania Umoja wa mataifa Geneva Balozi
Modest Jonathan Mero.
Balozi Masilingi-Uholanzi akiapa
Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (UAE) akiapa.
Balozi Mero-Geneva akiapa
Balozi Kilumanga-Commoro Akiapa
Marehemu Chinua Achebe kuzikwa leo Nigeria
Mwili wa mwandishi mashuhuri wa vitabu barani Afrika Chinua Achebe umewasili nyumbani kwake katika jimbo la Anambra nchini Nigeria.
Hafla mbali mbali zimekuwa zikiandaliwa nchini Nigeria kumuenzi bwana Achebe.
Mwandishi huyo mashuhuri alifariki mjini Boston,Marekani, akiwa na umri wa miaka 82 baada ya kuugua kwa muda mfupi. Jamaa na maafisa wa serikali walikuwa katika uwanja wa ndege Kusini mwa Nigeria kumpokea marehemu.
Hayati Achebe, anasifika sana kwa kuwa mwanzilishi wa fasihi ya kiafrika kwa kiingereza. Kitabu chake alichokianda cha kwanza, mwaka 1958, Things Fall Apart, ambacho kilizungumzia sana athari za ukoloni barani Afrika, aliweza kuuza zaidi ya vitabu milioni kumi.
Mwandishi huyo na msomi, aliendelea na uandishi wake na kuandika vitabu vingine 20 baadhi vikikosoa sana wanasiasa na kile alichokitaja kama ukosefu wa uongozi nchini Nigeria.
Alikuwa anaishi nchini Marekani tangu mwaka 1990 baada ya ajali ya barabarani kumjeruhi kiasi cha kumlemaza. Makundi ya kitamaduni yalifanya tamasha mbali mbali nje ya uwanja wa ndege wa Enugu, huku ndege iliyokuwa inambeba marehemu Achebe ilipotua.
Inaarifiwa kuwa licha ya kuwa watu wana majonzi tele, lakini pia wanasherehekea maisha ya mwandishi huyo. Achebe atazikwa karibu na nyumbani kwa familia yake mjini Ogidi, mji mdogo kwenye vilima vya jimbo la Anambra.Habari kwa hisani ya BBC Swahili.
GHANA, KENYA KUTINGA FAINALI GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE
Naab Jonathan Baan& Desmond Odaano: .Washindi wa kwanza wa nusu fainali ya kwanza ya Guiness Football Challengekutoka Ghana Naab Jonathan Baan(kushoto) na Desmond Odaano(kulia) katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Pan-Africa Guinness Football Challenge Larry Asego na Mimi Kalinda.
Francis Wangari& Kepha Kimani: Washindi wa pili wa nusu fainali ya kwanza ya Guiness Football Challenge Francis Wangari(kushoto) na Kepha Kimani(kulia) kutoka Kenya katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Pan-Africa Guinness Football Challenge Larry Asego na Mimi Kalinda.
======= ====== =======
Dar es Salaam: Jana usiku kupitia televisheni za ITV na Clouds TV nusu fainali ya kwanza kabisa ya GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ ilirushwa hewani na katika runinga Afrika nzima ambapo timu ya Ghana ilionesha ni kwanini ni timu bora ambayo ndiyo imejishindia pesa nyingi mpaka sasa.
Jonathan Nabb na Desmond Odaano walionesha uwezo na ujasiri wao walipoibuka washindi zidi ya wapinzani wao timu kutoka Kenya katika mchezo wa jana.
Katika hatua ya pesa ukutani walifanikiwa kulenga lango namba nne na hivyo kupata dola za kimarekani 12,000 wanazoziongeza katika dola 8,500 walizokuwa nazo awali katika hatua ya robo fainali.
Wakenya Francis Ngigi na Kepha Kimani ambao ni washindi wa pili katika nusu fainali hii wataungana na Ghana katika fainali. Ingawa waliikosakosa hatua ya ukuta wa pesa wa Guinness bado wana nafasi ya kuwa mabingwa katika fainali.
Wakulima sasa kupata taarifa za kilimo kupitia simu
Balozi wa Finland nchini Tanzania, Sinikka Antila akisalimiana na Afisa maendeleo ya Biashara wa Vodacom Tanzania Nixon Bonaventure wakati wa hafla ya kuanzisha Ushirikiano kati ya kampuni hiyo na kampuni ya Sibenonke ya nchini Finland. Pamoja nao katika picha ni Waziri wa Mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa Alexander Stubb (katikati). Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala ( wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe Schwarz. Hafla hiyo ilifanyika nyumbani kwa balozi huyo.
Waziri wa mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa wa Finland, Alexander Stubb, akifanya mahojiano na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Bw.Matina Nkurlu katika hafla ya kuingia katika Ushirikiano utakao wawezesha wakulima kupata taarifa za kilimo kupitia simu za mkononi. Pamoja nao ni Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala (wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe Schwarz.
India inajulikana kwa lipi zaidi?!
India inajulikana kwa lipi zaidi? Movies(Bollywood), shule bora au matibabu?? Sasa Airtel ya kuwezesha kulonga zaidi na walio india kwa bei nafuu,Kwa tsh 3000 tu utapata dakika 25, za kuwasiliana wiki nzima.
kujiunga piga*149*13# upate kuwasiliana kwa bei poa ya shilingi 2 kwa sekunde . Airtel Yatosha!!
majambazi yapora sayansi mataa-kijitonyama kweupeee jijini dar,risasi zarindima.
Pichani ndio matundu ya risasi zilivyorindima kwenye kioo cha dereva (risasi tatu) na kushoto risasi moja kama kionekanavyo kioo cha juu,mara majambazi hayo kufanikiwa kumjeruhi dereva sehemu ya bega na kufanikiwa kunyakua begi linalosadikiwa kuwa,lilikuwa na kiasi cha fedha shilingi milioni 40 na kutokomea nazo.
Pichani kulia ni Askari Usalama barabarani akichukuliwa maelezo yake kutokana kushuhudia tukio la ujambazi lililofanyika maeneo ya Sayansi mataa-Kijitonyama jijini Dar mapema leo mnamo majira ya saa tano kasoro.
Pichani kulia ni Askari Usalama barabarani akichukuliwa maelezo yake kutokana kushuhudia tukio la ujambazi lililofanyika maeneo ya Sayansi mataa-Kijitonyama jijini Dar mapema leo mnamo majira ya saa tano kasoro.
Ambapo kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio
wanaeleza kuwa majambazi hao walikuwa wapatao wanne wakiwa wamepanda
piki piki,ghafla wakasimama na kulizunguka gari aina Vitz yenye usajili
wa namba T929 CCX (pichani chini) kwa haraka,mmoja wao akiwa na mashine
gun na wengine walikuwa na bastola.
Mmoja wao alifyatua risasi hewani
kumtaka dereva asimame na ashushe vioo vya gari yake,kufuatia hali ya
utata wa majibishano ya muda mfupi majambazi hao waliifyatulia risasi
kadhaa gari hiyo upande wa dereva, bahati mbaya wakamjeruhi sehemu
ya bega,ndipo wakafanikiwa kuondoka na begi kubwa linalosadikiwa kuwa
lilikuwa na kiasi cha fedha shilingi milioni 40 (kwa mujibu wa dereva
aliempeleka majeruhi hospitali),mara baada ya majambazi hayo kutimka
wasamalia wema wakamchukua dereva huyo aliyekuwa akigugumia kwa maumivu
ya jeraha lake na kumtafutia tax na hatimae kumkimbiza hospitali ya
Kairuki kwa huduma ya haraka.
Baadhi ya watu wakijaribu kubadilshana mawazo kwa kulitafakari tukio hilo la ujambazi.
Gari iliyokuwa imevamiwa na majambazi ikikokotwa na gari la polisi mara baada ya kushindwa kuwaka.
DK. ASHA-ROSE ATAJA MAAZIMIO YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM
DODOMA, Tanzania.
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizungumza na waandishi wa habari leo, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Amezungumzia kuhusu yaliyojiri kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM, kilichofanyika jana, pia mjini Dodoma. (TAARIFA NA PICHA NA BASHIR NKOROMO
TAARIFA KAMILI KAMA ILIVYOTOLEWA NA DK. ASHA-ROSE
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya kikao chake cha kawaida mjini Dodoma Mei 21, 2013 chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu ilijadili na kutafakari masuala mbali mbali yanayohusu Uchumi, Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Taifa.
MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI
Migogoro ya wakulima na wafugaji imekuwa mingi na imeenea sana katika taifa letu. Migogoro hii inatokana na sababu nyingi: mabadiliko ya tabia nchi; ongezeko la idadi ya watu na mifugo. Kamati Kuu inasikitishwa na kuendelea kwa migogoro hii ambayo imekuwa tishio la amani na usalama katika jamii, na pia kusababisha wakulima kupata hasara baada ya mazao yao kuliwa na mifugo. Tumeishuhudia migogoro hii mkoani Morogoro hivi karibuni, katika ziara ya Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana na imeripotiwa katika maeneo mengine ya nchi yetu.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuishughulikia na kuitafutia ufumbuzi wa kudumu migogoro hii. Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuharakisha zoezi la kutenga maeneo kwa ajili ya wakulima na wafugaji na kujenga miundombinu ya malisho, maji, na majosho ili kuwezesha wafugaji kutohamahama na mifugo yao.
KULINDA HIFADHI
Kamati Kuu imezungumzia suala la mahusiano kati ya Hifadhi za taifa, wafugaji na wananchi waishio katika vijiji vinavyozunguka Hifadhi hizo. Kamati Kuu inatambua umuhimu wa Hifadhi kwa manufaa ya taifa letu na vizazi vijavyo. Inasisitiza msimamo wake wa kuzilinda Hifadhi za taifa sanjari na kuanzisha na kuendeleza mahusiano hayo.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuwashirikisha wananchi katika kutenga maeneo ya Hifadhi, kulinda maeneo ya wanyama pori na kutenga maeneo ya malisho ili kuondosha migogoro isiyo ya lazima katika maeneo yanayozunguka Hifadhi.
ZAO LA KOROSHO
Kamati Kuu ilijadili matatizo yanayolikabili zao la korosho ambayo ni: kuyumba kwa bei ya korosho, malipo ya wakulima kuchelewa, tozo nyingi wanazolipishwa wakulima na udhaifu wa baadhi ya vyama vya ushirika.
Tatizo hili limedumu kwa muda mrefu na linastahili kushughulikiwa kwa njia ya kipekee.
Kwa kutambua kwamba wapo baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali, viongozi wa vyama vya ushirika na wafanyabiashara binafsi wanaochangia katika kuendeleza matatizo yanayowakabili wakulima wa korosho:
Kamati Kuu inatamka kwamba hali hii haivumiliki. Kamati Kuu inaitaka Serikali kukaa na wadau wote na kuchukua hatua zitakazotoa ufumbuzi wa kudumu wa matatizo haya kwa zao la korosho. Kamati Kuu pia inaitaka Serikali kuwachukulia hatua za kisheria hao wote wanaochangia kuendelea kwa matatizo haya kwa wakulima wa korosho.
MIGOGORO YA KIDINI
Kamati Kuu imepokea taarifa ya namna migogoro ya kidini inavyoshughulikiwa na hatua zinazochukuliwa. Kamati Kuu inaipongeza Serikali na vyombo vya dola kwa namna inavyoendelea kukabiliana na wahalifu wanaotumia mgongo wa dini kuanzisha vurugu na uvunjifu wa amani katika nchi yetu. Kamati Kuu inatoa mwito kwa Watanzania kukataa vitendo vyote vinavyochochea migogoro ya kidini; wananchi wajihadhari na watu waovu wenye nia mbaya ya kuligawa taifa letu.
Pamoja na jitihada za vyombo vya dola hadi sasa, Kamati Kuu inaitaka Serikali iandae mkakati wa kuzuia migogoro ya kidini kabla haijajitokeza.
MAKAMPUNI NA VIWANDA VILIVYOBINAFSISHWA
Kamati Kuu imetafakari hali ya viwanda hivi. Ni muongo mmoja umepita tangu ubinafsishaji ulipokamilika. Kuuzwa kwa mashirika na viwanda vya umma kwa watu na makampuni binafsi kumekuwa na matokeo ya aina mbili: yako yale yaliyobinafsishwa na yakawa na maendeleo mazuri na kuchangia uchumi wa Taifa. Na yako ambayo yanaendeshwa kwa kiwango cha chini au yamefungwa.
Kamati Kuu inasikitishwa na hali hii, kwani viwanda vilivyofungwa ni vile vilivyokuwa vikifanya kazi muhimu ya uzalishaji.
Viwanda hivi ni vya korosho, usindikaji wa pamba, mafuta ya kula, viwanda vya mazao ya ngozi, na vinginevyo. Hali hii inalikosesha Taifa fursa za ajira, kukua kwa mapato, kuimarika kwa uzalishaji na kuongezeka kwa uuzaji wa bidhaa zilizosindikwa na kuzalishwa nchini.
Imedhihirika kuwa wafanyabiashara waliochukua viwanda hivyo ndiyo hao hao wanaofanya biashara ya kununua mazao ya kilimo na mifugo na kuuza nje kama bidhaa ghafi, wakati huo huo wakiwa wamevifunga viwanda hivi.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kufanya tathmini ya viwanda vilivyobinafsishwa ili kuvitambua vile vilivyofungwa, na kuwataka waliouziwa wavifungue na iwapo watashindwa kutimiza masharti yaliyowekwa, Serikali iandae utaratibu wa kuwapa watu wenye uwezo wa kuviendesha.
WAKULIMA WADOGO WA MIWA -
Kumekuwapo na migogoro ya muda mrefu kati ya wakulima wadogo wa miwa na Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa mkoani Morogoro. Matatizo haya yameshughulikiwa na watendaji mbalimbali bila ya kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kuushughulikia mgogoro huu na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya wakulima wadogo wa miwa haraka iwezekanavyo.
PEMBEJEO ZA KILIMO.
Chama kimejiridhisha kuwa suala la utoaji wa pembejeo za kilimo ni zuri na lenye mafanikio. Hata hivyo Kamati Kuu imepokea taarifa kuhusu matatizo yanayohusiana na usambazaji wa mbolea ya ruzuku.
Kwa baadhi ya maeneo mbolea ya ruzuku imekuwa ikitolewa kwa watu wasiohusika na wakati mwingine walanguzi wamekuwa wakiingilia kati ili kujinufaisha nayo.
Kamati Kuu inaiagiza Serikali kusimamia kwa umakini na kutafuta utaratibu bora zaidi na wenye tija wa kuwafikishia wakulima mbolea, kwa wakati na kwa uhakika.
MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI.
Kamati Kuu imepokea taarifa na kuipongeza Serikali kwa kutayarisha mpango kabambe wa ujenzi wa nyumba za watumishi wake. Mpango huu utatoa fursa kwa wafanyakazi ya kupata mikopo yenye masharti nafuu na hivyo kuwawezesha kuwa na makaazi yenye uhakika.
MWISHO:
Kamati Kuu imeitaka Serikali kuwasilisha utekelezaji wa maagizo haya mara kwa mara.
IMETOLEWA NA:
Asha-Rose Migiro,
Katibu WA NEC – Siasa Na Uhusiano wa Kimataifa,
Mei 22, Dodoma.








.jpg)









.jpg)








.jpg)
